Orodha ya maneno ya TEHAMA na tafsiri zake!…

Habari!, najua kwa sasa Tekinolojia ya Habari na Mawasiliano inashika hatamu nchini mwetu na hii inafanya watu wengi wapende kutumia vifaa kama kompyuta na simu za mkonnoni ili wasiwe nyuma. Pamoja na hayo bado kuna ugumu wa kutumia na kufurahia teknolojia hii, achilia mbali athari ambatanishi zinazoweza kusababishwa na kutokuelewa lugha inayotumika ambayo ni kiingereza, pia hata kiswahili chake kinaonekana kuwa kigumu sana kwa watumiaji wapya na hata wale ambao walishazoea kutumia kompyuta kwa kiingereza.

Mimi kama mdau wa TEHAMA inchini bado nina hamu ya kuona Watanzania wenzangu wakuwa huru na kujivunia kutumia kompyuta kwa lugha yao kama wanavyotumia wenzetu.

Kuna faida nyingi sana ukijaribu kutadhmini hili. hata hivyo ugumu wa kiswahilli chenyewe kiapelekea hata waandaaji wa programu za kompyuta kushindwa kuweka maneno sahihi na marahisi kwenye programu zao. Mfano neno password ambalo kwa tafsiri halisi ni neno ambalo mtumiaji atatakiwa kuliandika kabla hajapata ruhusa ya kufanya jambo fulani katika mfumo wa kikompyuta limekuwa na tafsiri mbili kinzani ambapo mwisho wa siku mtumiaji ataamua kusema password ni nenosiri, wakati wanazuoni wanasisitiza kuwa password tafsiri yake ni nywila, sasa wangapi kati yetu tulikuwa tunalifahamu neno hili?

Bila kukuchosha, ningependa upakue faili hili na upate kufahamu baadhi ya maneno ya tehama na tafsiri zake. Maneno hayo yanaweza kuwa rejea yako endapo utahitaji kufahamu zaidi neno fulani pindi ukikutana nalo.

Bofya hap Kupakua Faili lenye Orodha ya maneno

© 2024, WEBNERD SOLUTIONS